Vichwa vya habari vya magazeti ya leo tarehe 2 Februari 2016 kutokea ndani ya #NDT Newsroom




Rais Magufuli Amhamisha Mlawi Kwenda Wizara ya Ofisi ya Rais


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemhamisha Bi. Suzan Paul Mlawi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Manejimenti ya utumishi wa umma na Utawala Bora.
Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, imeeleza kuwa uhamisho huo umeanzia tarehe 26 Januari, 2016.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa pamoja na shughuli nyingine za Unaibu Katibu Mkuu, Bi. Suzan Paul Mlawi, atashughulikia eneo la Utawala Bora.
Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria iliyoachwa wazi, haitajazwa kwa sasa.

Zitto Ataka Bunge Liachwe Huru


Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe ameiomba serikali kupitia Bunge lake la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuacha kufanya kazi kwa matakwa ya watanzania wachache na kuwaacha watazania wengi ambao ni walipa kodi kwenye mamatizo.
Ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa akizungumza na East Africa Radio wakati akifafanua kile kinachoendelea kwa sasa Bungeni na kuwaomba wabunge wenzake kuhakikisha wanasimamia haki ya kikatiba katika kutafuta maendeleo ya nchi na kuongeza pato la taifa.
Amesema kuwa watanzania wengi wanategemea wawakilishi wao ambao ni wabunge waliowachagua kidemokrasia kuwafikishia matatizo yao serikali kupitia Bunge kwa lengo la kuwasaidia na kuyatatua matatizo yao ndani ya kijamii zao.
Aidha Mhe. Zitto amesema kuwa haipaswi bunge kubanwa kitu ambacho kitaminya demokrasia, hivyo ni vyema bunge likaachiwa huru lifan

Davido kusheherekea dili lake la Sony kwa kutoa pesa kwa shabiki.


Staa wa muziki kutoka Nigeria atatoa Naira milioni 2 kwa shabiki kama sehemu ya kusheherekea dili lake la Sony la dola milioni moja.
Davido ambaye yuko mjini New York ameahidi kufanya sherehe mbili kubwa kama asante kwa mashabiki kwa dili lake la Sony Music na kuumpa naira milioni 2 shabiki wake wa ukweli.
” Doin two signing parties in Nigeria when I get home … I’m giving my most loyal fan 2 MILLION NAIRA !! “

DUKA LA VIFAA VYA SIMBA LAFUNGULIWA DAR

Klabu ya Simba Sports February 1 2016 imeingia kwenye headlines na historia, baada ya uongozi wa klabu hiyo kupitia kwa Rais wa klabu hiyo Evans Aveva wamezindua duka ambalo litakuwa linauza vifaa vyenye nembo ya klabu hiyo, hili ndio duka la kwanza rasmi la Simba kufunguliwa.Baada ya hapo Rais wa Simba Evans Aveva amethibitisha kufungua duka jingine la bidhaa za klabu katika makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi Kariakoo siku za hivi karibunia. Simba sasa imepiga hatua moja mbele na kuiga mfano wa vilabu vya Ulaya kama FC Barcelona ambavyo vinamiliki maduka ya bidhaa zenye nembo ya klabu yao.

WATUMISHI 508 WA MAHAKAMA KUCHUKULIWA HATUA ZA KINIDHAMU ASEMA JAJI MKUU MHE. MOHAMED OTHMAN CHANDE.

jajiJaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Othman Chande amesema kuwa Mahakama ya Tanzania itawachukulia hatua za kinidhamu na za kisheria Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo,Wilaya na wale wa Mahakama za Hakimu Mkazi wapato 508 kote nchini waliotekeleza majukumu yao chini ya kiwango na kushindwa kutimiza wajibu wa Mahakama wa Utoaji wa Huduma Bora kwa wananchi katika mwaka wa Sheria wa 2015/2016.
Akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam alipokua akitoa ufafanuzi kuhusu  kuanza kwa mwaka mpya wa Sheria wa 2016 na Maadhimisho ya Wiki ya Sheria ambayo kilele chake kitakua Januari 4,2016 Jaji Mkuu amesema  kuwa kwa mujibu wa taratibu za uendeshaji wa Mahakama na upimaji wa viwango vya utendaji kazi vilivyowekwa, Mahakimu hao wa Mahakama za wilaya na Hakimu Mkazi 121 na 387 wa Mahakama za Mwanzo watatakiwa  kutoa maelezo ndani ya siku 7 juu ya sababu zilizowafanya washindwe kutimiza lengo lililowekwa la kushughulikia mashauri 260 kila mmoja.
Amesema watakaothibitika  kamati za nidhamu na maadili za kila wilaya na Mikoa ambazo ni Kamati ndogo za Tume ya Utumishi wa Mahakama zitawafungulia kesi za kinidhamu ndani ya siku 21.
“Wale watakaobainika watakumbwa na adhabu ya kupewa Onyo, kushushwa vyeo na kufukuzwa kazi ili iwe fundisho kwa wengine, ninajua wapo baadhi ambao waliajiliwa katikati ya mwaka, wengine kwenda mafunzo ya vitendo vyuoni, wajawazito na baadhi vituo vyao kuwa na kesi chini ya 260 kwa mwaka” Amesisitiza.
Aidha, katika hatua hiyo amewapongeza Mahakimu waliofanya vizuri katika utendaji wao wakiwemo 14 walioshughulikia mashauri zaidi ya 700 kila mmoja, Mahakimu 50 walioamua kesi zaidi ya 500 kila mmoja baadhi wakitokea wilaya ya Mkuranga, Rufiji  na Bukoba mjini na wengine wawili kutoka Dar es salaam walioamua kesi zaidi ya 900 kila mmoja na  kuvuka lengo la utendaji lililowekwa la kushughulikia mashauri 260 kwa mwaka.
Akitoa tathmini ya utendaji wa Mahakama kwa mwaka wa sheria uliopita amesema kuwa Mahakama ya Tanzania ina Mahakama za Hakimu Mkazi kila Mkoa na Mahakama za Wilaya 111 katika wilaya za Kiserikali 133 pamoja na Mahakama za Mwanzo ambazo hupokea asilimia 93 ya mashauri yanayofunguliwa kote nchini.
 Amesema mwaka 2015 Mahakama zote nchini zilipokea jumla ya mashauri 206,115, kati ya hayo mashauri 220,815 yaliamuliwa kukiwa na ziada ya mashauri 14700 jambo linaloonyesha kuwa Mahakama zinapokea mashauri na kuyashughulikia kwa kasi inayoridhisha huku mashauri yanayosababisha mrundikano ni yale yaliyo nje ya idadi iliyopangwa.
Ameongeza kuwa katika katika kipindi cha mwaka huo wa 2015 Mahakama za Mwanzo zilipokea mashauri 141,025 ambapo kati ya hayo Mashauri 149,757 yalishughulikiwa huku idadi ya Mahakimu walioshughulikia mashauri hayo ni 1240.
“Ukiangalia mwenendo wa ufunguaji wa mashauri yote kote nchini hasa Tanzania Bara utagundua kuwa Mahakama za Mwanzo, Wilaya na zile za Hakimu Mkazi  zinapokea mashauri mengi kwa asilimia 93 ,katika kila mashauri 4 yanayofunguliwa nchini 3 yako mahakama za mwanzo ambako wananchi wengi wanatafuta ufumbuzi wa kesi zao lazima tuweke mkazo” Amesema Jaji Mkuu.
Kuhusu kuanza kwa mwaka mpya wa Sheria mwaka 2016 amesema Mahakama inauanza chini ya Kauli Mbiu Isemayo “Huduma Bora kwa Wananchi ni Wajibu wa Mahakama na Wadau wake”  ikiwa na kesi 20,431 ikilinganishwa na 34,126 ilizoanza nazo mwaka 2015 na kuongeza kuwa licha ya changamoto zinazoikabili Mahakama ya Tanzania mkakati uliopo ni kupunguza idadi hiyo hadi kufikia 0 kwa kila mwanzo wa mwaka wa sheria.
Akitoa ufafanuzi kuhusu upatikanaji wa Nakala za hukumu amesema Serikali inaendelea kuijengea uwezo wa kifedha Mahakama wa kuajiri wachapaji wa nakala wengi zaidi ili Nakala za Hukumu za Kesi ziweze kupatikana pindi tu kesi zinapomalizika katika mahakama zote nchini tofauti na ilivyo sasa ambapo hupatikana Mahakama Kuu na Mahakama za Rufani.
Aidha, amesema Mahakama inaendelea kuboresha miundombinu yake ikiwemo majengo na ujenzi wa mahakama mpya katika maeneo yasiyo na huduma hiyo katika mwaka 2016. “ Hivi sasa tuna wilaya 23 hazina Majengo ya Mahakama za wilaya, kwenye baadhi ya maeneo kesi zinasikiliziwa Ofisini kwa Hakimu wakati ilitakiwa ziwe kwenye jengo lenye ukumbi wa wazi,tumejiandaa kwa michoro ya majengo kwa mahakama zote ili tuanze kujenga kwa gharama nafuu”  
Mhe. Chande ametoa wito kwa wananchi kutosita kuitumia Mahakama ya Tanzania katika kupata ushauri wa kisheria kupitia wataalamu wake, kuhudhuria maonesho mbalimbali ya kisheria yanayofanyika nchini huku akitoa angalizo kwa baadhi ya watu wanaochangia kuwepo kwa mrundikano wa kesi kwa kufungua kesi za madai au kupeleka mashauri Mahakamani kama sehemu ya maegesho ya masuala yao.
“Baadhi ya watu wamekuwa wakipeleka kesi Mahakamani kama sehemu ya maegesho, huzifungua kisha hushindwa kujitokeza Mahakamani hizi ni tofauti na zile zenye vipengele vingi ndani ya kesi moja au zile ambazo mashahidi wake wamehama kutoka eneo moja kwenda linguine, hizi nawahakikishia tutazifuta ili kupunguza mrundikano wa kesi kwenye Mahakama zetu” Amesisitiza Mhe. Chande.
©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved