MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AMUWAKILISHA RAIS KIKWETE KUSAINI MAKUBALIANO YA KUWA NA SOKO LA PAMOJA KWA NCHI ZA WANACHAMA WA KANDA YA TATU YA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI, KUSINI MWA AFRIKA NA ZA MAGHARIBI.

1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini mkataba wa makubaliano ya kuwa na soko la pamoja kwa Nchi za Wanachama wa Kanda ya tatu ya Nchi za Afrika Mashariki, Kusini mwa Afrika na za Magharibi. Dkt.Bilal pamoja na Viongozi wa Nchi husika wamesaini mkataba huo leo katika Mkutano mkuu wa tatu wa Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Soko la pamoja la Nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Sharm El Sheikh, nchini Misri.
Picha zote na OMR
3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo na Waziri wa Afrika Mashariki, Dkt. Harrison Mwakyembe, akimpongeza baada ya kusaini mkataba huo.

5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa na baadhi ya Mawaziri wake katika mkutano mkuu wa tatu wa Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Soko la pamoja la Nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika leo Juni 10, 2015 kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Sharm El Sheikh, nchini Misri.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved