
Wengine waliotoa kauli jana ni Amina Salum Ali
ambaye amewaponda wanaoamini kuwa wanawake hawawezi kuwa viongozi,
Samuel Sitta aliyesisitiza kutaifisha mali za mafisadi na Steven Wasira
ambaye amelia kuchezewa rafu ili aenguliwe kwenye kinyang’anyiro.
Ushauri wa Mwandosya
Profesa Mwandosya alisema utaratibu wa kuanza
kumchagua mgombea wa kiti cha urais kabla ya mwenyekiti wa chama ni
mbovu na ndiyo unaosababisha msururu wa watu kutaka kuwania nafasi hiyo
ya juu serikalini.
“Kwa maoni yangu tungeanza kwanza kumpata
mwenyekiti wa chama, kabla ya mgombea urais na hii ingesaidia kupunguza
idadi ya makada wa CCM wanaotaka kuwania urais. Idadi ya watu 30
walijitokeza kutangaza nia ingepungua sana, lakini sasa hatuwezi
kuvuruga utaratibu uliopo,” alisema alipowasili mkoani Geita kutafuta
wadhamini. Profesa Mwandosya aliyekuwa ameongozana na mkewe na mtoto
wake mkubwa, Max na Katibu wa Siasa na Uenezi Mkoa wa Mbeya, Bashiru
Madodi aliwasili mkoani Geita saa tano asubuhi akitokea mkoani Mwanza.
Wanawake wanaweza
Amina ambaye kwa sasa ni Balozi wa Umoja wa Afrika
(AU) alisema watu wanaowabeza wanawake kugombea uongozi kwa madai kuwa
hawawezi, wana mawazo mepesi na kusahau kuwa wapo wengi walioongoza
mataifa makubwa na wengine ambao bado wanashikilia nafasi za juu katika
nchi zao.
Alitaja nchi ambazo kuna viongozi wa juu wanawake
kuwa ni Liberia na Ujerumani na kukumbushia michango ya wanawake kama
Benazir Butto, Margareth Thatcher na Indira Gandi.
Alisema Mwanamke ndiye anayeguswa na matatizo
mbalimbali katika jamii, ikiwamo ya afya, umaskini, elimu na usimamizi
wa familia, kwa vile ndiyo anayokabiliana nayo mara kwa mara katika
maisha ya kila siku ya Watanzania.
“Dhana ya mwanamke hafai kuongoza taifa, imepitwa
na wakati na inabidi wanaopinga warudi kwenye historia na kupekua
kumbukumbu za viongozi wanawake waliopata mafanikio wakati wakiziongoza
nchi zao,” alisema.
Sitta kutaifisha mali za mafisadi
Akizungumza muda mfupi baada ya kukamilisha ziara
yake ya kuzuru kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dk Omar Ali Juma katika Kijiji cha Wawi, Mkoa wa Kusini
Pemba, akiwa ameambatana na wana-CCM kadhaa, Sitta ambaye ni Waziri wa
Uchukuzi aliapa kutaifisha mali za viongozi wote zilizopatikana kwa njia
haramu na kuhujumu uchumi, iwapo chama chake kitamteua kuwa mgombea
urais. “Kama nikijaliwa kufika katika safari yangu, sheria moja kali
itakuwapo, kwamba kiongozi mwenye mali isiyoelezeka, basi kwa kiwango
kilekile tutaitaifisha,” alisema Sitta.
No comments:
Post a Comment