Pwani waanza kujiandaa kujiandikisha BVR

Mkuu wa mkoa wa PWANI Mhandisi EVARESTI NDIKILO
Mkuu wa mkoa wa PWANI Mhandisi EVARESTI NDIKILO amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa huo kuwamakini wakati wa zoezi la kuandikisha vitambulisho vya kupigia kura litakapoanza jumapili wiki ijayo ili kuhakikisha watu watakaoadikwa ni raia wa Tanzania.

Mhandisi NDIKILO ametoa rai hiyo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa wataalamu kutoka ngazi ya wilaya watakaoratibu zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya kupigiakura mwa mpya wa BVR.

Naye mwenyekiti wa wakurugenzi katika mkoa wa PWANI JENIFA OMOLO amemhakikishia mkuu wa mkoa kuwa halmashauri zote zimejipanga kusimamia vyema zoezi hilo ili kila mtanzania mwenye umri wa kupiga kura awe amejiandikisha bila usumbufu.

Zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la mpiga kura katika mkoa wa pwani litaanza Rasmi June 14 mwaka huu na litadumu kwa muda wa siku thelathini.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved