Kiongozi Muadhamu: Vikwazo dhidi ya Iran viondolewe

http://static.iqna.ir/19/news/201504/85877296062088654721571840400.jpgKiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema kuhusiana na mazungumzo ya nyuklia ya Iran na kundi la 5+1 kwamba, vikwazo vya kiuchumi, kifedha na kibenki dhidi ya taifa hili vinapaswa kuondolewa mara moja wakati wa kutiwa saini makubaliano na kwamba, kuondolewa vikwazo hivyo, hakupaswi kufungamanishwa na utekelezaji wa ahadi za Tehran. Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei amesema hayo alasiri ya jana wakati alipokutana na viongozi na maafisa wa mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ambapo alibainisha wazi mistari myekundu ya nyuklia ya Iran na kusisitiza kwamba, Wamarekani wanataka kuangamiza teknolojia ya nyuklia ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema bayana mbele vya viongozi na maafisa wa mfumo wa Kiislamu hapa nchini kwamba, Iran inafuatilia kuhakikisha kwamba, kunapatikana makubaliano mazuri yaani makubaliano ya kiadilifu, kiinsafu, ya heshima na ambayo yanakwenda sambamba na maslahi ya taifa hili. Ayatullah Khamenei amesema kuwa, taifa hili tofauli na wanavyong'ang'ania Wamarekani, halikubaliani na uwekaji mipaka wa muda mrefu wa miaka 10 hadi 12 na kubainisha kama ninavyomnukuu: 'kiwango cha miaka ambayo inakubalika tumekwishawaeleza Wamarekani.' Mwisho wa kunukuu.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved