Dyke amesema hakuna njia ya kurejesha imani kwa FIFA wakati Blatter akiwa bado yupo, na kuonegeza kuwa lazima aondoke kwa kujiuzulu, kupitia uchaguzi au watafute njia ya tatu. Shirikisho hilo la kandanda limetumbukia katika mgogoro wakati likijiandaa kuchagua rais mpya, likishtumiwa na serikali ya Marekani kwa uozo. Maafisa saba walikamatwa katika uvamizi wa alfajiri kwenye hoteli ya kifahari mjini Zurich, na kutuhumiwa kwa kuchukuwa zaidi ya dola milioni 150 katika hongo, huku maafisa wengine 14 wa FIFA na watafuta masoko wakituhumiwa kwa shughuli haramu, udanganyifu na usafirishaji haramu wa fedha. Blatter amekuwa akishika usukani wa FIFA tangu mwaka 1998, na amenusurika na kashfa kadhaa zikiwemo kuhusu madai ya rushwa, katika utoaji wa zabuni za uenyeji wa mashindano ya kombe la dunia, kwa Urusi mwaka 2018 na Qatar mwaka 2022.
Mwenyekiti FA ataka Blatter aondolewe kwa njia yoyote ile
Dyke amesema hakuna njia ya kurejesha imani kwa FIFA wakati Blatter akiwa bado yupo, na kuonegeza kuwa lazima aondoke kwa kujiuzulu, kupitia uchaguzi au watafute njia ya tatu. Shirikisho hilo la kandanda limetumbukia katika mgogoro wakati likijiandaa kuchagua rais mpya, likishtumiwa na serikali ya Marekani kwa uozo. Maafisa saba walikamatwa katika uvamizi wa alfajiri kwenye hoteli ya kifahari mjini Zurich, na kutuhumiwa kwa kuchukuwa zaidi ya dola milioni 150 katika hongo, huku maafisa wengine 14 wa FIFA na watafuta masoko wakituhumiwa kwa shughuli haramu, udanganyifu na usafirishaji haramu wa fedha. Blatter amekuwa akishika usukani wa FIFA tangu mwaka 1998, na amenusurika na kashfa kadhaa zikiwemo kuhusu madai ya rushwa, katika utoaji wa zabuni za uenyeji wa mashindano ya kombe la dunia, kwa Urusi mwaka 2018 na Qatar mwaka 2022.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment