Ombi likapokelewa kwenye meza ya Naibu Spika leo June 26 2015 >>>”Nimepokea ombi maalum la kuwasilisha maombi binafsi kutoka kwa Mbunge Joseph Mbilinyi kwa hiyo namruhusu” >>> Naibu Spika Job Ndugai.
“Asante
sana Naibu Spika, naomba nitoe maelezo binafsi jana tarehe 25 June 2015,
Mbunge Martha Mlata alidai kuwa kuna Mbunge wa CHADEMA amempora
mwanamke mmoja mtoto mdogo wa miaka miwili na amempora wakati Mbunge
huyo amekuwa hatoi matunzo kwa mama yake… Mlata aliwataka Wabunge wote
wanawake kuungana kukemea kitendo alichodai kimefanywa na Mbunge huyo”
“Asante
sana Naibu Spika, naomba nitoe maelezo binafsi jana tarehe 25 June 2015,
Mbunge Martha Mlata alidai kuwa kuna Mbunge wa CHADEMA amempora
mwanamke mmoja mtoto mdogo wa miaka miwili na amempora wakati Mbunge
huyo amekuwa hatoi matunzo kwa mama yake… Mlata aliwataka Wabunge wote
wanawake kuungana kukemea kitendo alichodai kimefanywa na Mbunge huyo”
“Hakutaja
jina la Mbunge aliyemhusisha na madai yake ila alidai kuwa ni msanii
mwenzake… hata hivyo alitaja jina la mwanamke anayedaiwa kunyang’anywa
mtoto kuwa ni Faiza. Mbunge aliyelengwa na mashambulizi ni mimi Joseph
Osmond Mbilinyi, mimi ndiye baba wa mtoto Sasha Desderia Mbilinyi
anaedaiwa kuporwa kwa mama yake, na Faiza aliyetajwa ni Faiza Abdallah
Ally ambaye ni mzazi mwenzangu na mama mzazi wa Sasha Desderia“
“Watu
wazima hawapendelei kuzungumzia mambo binafsi hadharani… Nadhani
sitakosea kusema hata Mheshimiwa Martha mwenyewe asingependa kuzungumzia
matatizo yaliyopelekea ndoa yake kuvunjika“
“Mimi ni mmoja wa watu wazima wenye akili
timamu ndio maana sijazungumzia hadharani kuhusu uhusiano wangu na mzazi
mwenzangu Faiza Ally na mtoto wetu Sasha… Sasha ameishi na mama yake
tangu alipozaliwa mwaka 2012, katika kipindi chote nimempelekea mama
yake laki tano kila mwezi, nimemlipia ada ya shule Milioni 3 kila
mwaka.. Mlata kama angekuwa anataka kujua angeniuliza ningempatia
taarifa hizi kabla hajarusha tuhuma nzito
““Mwanamke anayedaiwa kuwa mnyonge
anajulikana katika kumbi za starehe nchi nzima, picha zake zilisambazwa
katika Mitandao ya Kijamii na kuleta fedheha kubwa kwa watu wanaojali
maadili ya mavazi, picha zake nyingine akiwa amevaa diapers zilisambaa
mitandaoni na Martha Mlata angeweza kupata ukweli wa mambo haya kabla
hajarusha tuhuma mbele ya Bunge“
No comments:
Post a Comment