Pigo jingine CCM: Mbunge Eugene afariki Dunia, bunge lahairishwa



Mbunge wa jimbo la Ukonga Dar es Salaam kupitia tiketi ya (CCM) Eugen Mwaiposa amefariki dunia usiku wa kuamkia leo akiwa usingizini nyumbani kwake Dodoma.

Kwa mujibu wa Naibu Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai ambaye amelitangazia bunge leo majira ya saa 7 mchana, marehemu Mwaiposa alikuwa akisumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu kwa muda mrefu.

Ndugai amesema kuwa kwa sasa msiba upo nyumbani kwake eneo la Chadulu Dodoma ambapo pia familia yake inasubiria hapo kwa ajili ya kuaga mwili wake shughuli ambayo itafanyika kesho (Jumatano).

Bunge limeahirishwa hadi keshokutwa saa 3 Asubuhi.

Mungu ametoa Mungu ametwaa jina lake lihimidiwe. R.I.P ‪

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved