Habari ambazo mashabiki wa Manchester United wamekuwa wakihofia kuzipata
hivi karibuni hatimaye zimekuwa kweli baada ya kipa namba moja wa klabu
iyo Mhispania David De Gea kuiambia klabu hiyo kuwa anataka kuhamia
Real Madrid . De Gea kupitia wakala wake ameiarifu United kuwa dhamira
yake ni kujiunga na Madrid na amefikia uamuzi huo baada ya kipindi
kirefu cha kuwaza na kuamua ni hatua ipi bora ya kufuata kwenye
mustakabali wake . De Gea amekaa na United kwa muda wa miaka minne
tangu aliposajiliwa toka Atletico Madrid kwa ada ya uhamisho ambayo
iliweka rekodi kwa makipa ya paundi milioni 17 na amekaa United kwa muda
wa miaka minne , muda ambao amepia hatua kubwa kiasi cha kufikia kuwa
na kiwango cha ubora wa dunia . Hivi karibuni De Gea alipewa ofa ya
kuongezewa mshahara mpaka kufikia paundi 200,000 kwa wiki ofa ambayo
hajaikubali akiwa amefikia uamuzi wa kurudi nyumbani kwao kwenye mji
aliozaliwa na kukulia huku akipata fursa ya kuwa karibu na mpenzi wake
Edurne . De Gea amekuwa kwenye mipango ya Real Madrid kwa muda mrefu
ambapo klabu hiyo imemuweka kama chaguo namba moja la kuziba nafasi ya
mkongwe Iker Casillas ambaye umri wake unazidi kuwa mkubwa . Endapo
usajili huu wa David De Gea kuondoka United na kuhamia Hispania kwenye
uwanja wa Santiago Bernabeu , kipa huyo atakuwa mchezaji wa tano
kuondoka United baada ya Cristiano Ronaldo , David Beckham , Ruud Van
Nistelrooy na Gabriel Heinze. Klabu ya Manchester United ya nchini England imetangazwa kuwa klabu
yenye thamani kuliko zote duniani kufuatia utafiti uliondeshwa katika
kipindi cha miezi 12 iliyopita , utafiti uliohusisha klabu kubwa za soka
duniani .
Thamani ya United imeongezeka maradufu kutokana na mikataba kadhaa ya
udhamini na biashara ambayo imekuwa ikiingia kila mara chini ya uongozi
wa Mkurugenzi wa klabu hiyo Ed Woodward .
Chini ya uongozi wake thamani ya United imekuwa kubwa hali ambayo
imefanya timu hii kuwa na fedha ambazo zinaipa kiburi cha kuwa na uwezo
wa kufanya usajili wa nguvu bila kuhofia minyororo ya kanuni ya
financial fair play .
United inafuatiwa na klabu za Bayern Munich na Real Madrid ambazo
zimefuatana katika orodha kwenye nafasi ya pili na ya tatu huku
Manchester City na Chelsea zikikamilisha orodha ya 5 bora .
Fc Barcelona ambayo ubingwa wa ulaya iliyoutwaa juzi umeiongezea
kipato cha paundi milioni 28 iko kwenye nafasi ya sita nyuma ya Man City
.
Sababu kubwa ya kupanda kwa thamani ya Manchester United ni
Mkurugenzi wake Ed Woodward ambaye chini ya uongozi wake klabu hii
imeingia mikataba mingi yenye thamani kubwa .
No comments:
Post a Comment