Jk, Babu Seya Kuonana Uso Kwa Uso.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’, leo katika Viwanja vya Chuo cha Magereza ya Ukonga jijini Dar, ana ratiba ya kuzungumza na maafande na maafisa wa jeshi la magereza na wafungwa katika Siku ya Magereza Tanzania 2015 ambayo huadhimishwa kila mwaka.
Kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya jeshi hilo, pia Rais Kikwete atatumia nafasi hiyo kuliaga jeshi hilo kwa vile Oktoba, mwaka huu, nchi itamchagua rais atakayepokea kijiti chake cha urais kwa awamu ya tano.
Msingi wa habari hii ni wafungwa wanaotumikia kifungo cha maisha jela kwa makosa ya ulawiti na ubakaji, wanamuziki Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na mwanaye, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ kwani katika hafla kama hiyo, mwaka jana, walimtumia salamu JK wakimwomba awasamehe kwani walishatambua makosa yao.
“Je, rais hawezi kuitumia nafasi hiyo kuwaachia huru wanamuziki, Nguza Vicking na mwanaye, ‘Papii Kocha’ ambao wanatumikia kifungo cha maisha jela?
Chanzo: “Mh! Sina hakika sana. Maana kama hilo lipo ina maana ni jukumu la rais mwenyewe na mipango yake kwa mujibu wa katiba, rais ana mamlaka ya kumsamehe mfungwa kwa kosa lolote lile.”

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved