Kwa mara ya kwanza video ya Ali Kiba inaoneshwa kesho kwenye TV

Ali Kiba  ni staa mwingine mkali wa muda mrefu kwenye Bongo Fleva… Hit ya Chekecha Cheketua ni moja ya single ambazo mtaani wanaisubiri video yake kwa hamu sana.
Sasa good news ninayotaka kukusogea ni kwamba video hiyo mpya iliyotayarishwa Afrika Kusini inatarajiwa  kutambulishwa kesho June 29 kama ‘Exclusive’ kupitia kituo cha TV cha ufaransa maarufu kama Trace TV  kinachoonekana Africa kwa huduma ya kulipia kikiwa na nafasi yake kwenye upande wa burudani hususani muziki wa kizazi cha sasa.
Kupitia kwenye ukurasa wa instagram #TraceTV ya nigeria wamepost cover ya utambulisho wa video hiyo mpya na kuandika…’Catch the Video Premiere of ‘Chekecha Chekatua’ by Alikiba (@officialalikiba) on TRACE Urban on Monday at 9:23 am!!! #tanzania #worldpremiere #newvideo..

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved