RAIS JK AFAGILIA MAGEREZA DAY..;

Rais Dk. Jakaya Kikwete akipokea heshima ya Wimbo wa Taifa mara baada ya kuwasili katika Viwanja  vya Chuo cha Maofisa Magereza kilichopo Ukonga jijini Dar.

Rais JK akimpandisha cheo mwanafunzi bora katika kozi ya 21 kutoka Inspekta na kuwa ASP.

RAIS  wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Amiri Jeshi  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amelisifia Jeshi la Magereza kwa jitihada zao nzuri katika utendaji kazi pamoja na chagamoto nyingi walizonazo.
JK aliyasema  hayo  jana  katika shereha za Siku ya Magereza nchini ambapo  sherehe hizo kitaifa  zilifanyika kwenye Viwanja  vya Chuo cha Maofisa Magereza kilichopo Ukonga jijini Dar es Salama na  rais ndiye alikuwa mgeni rasmi.
Katika sherehe hizo,  Rais JK aliwapandisha maofisa 104 ambao walikuwa wakifanya mafunzo kutoka cheo cha Inspekta na kuwa ASP ambapo kati ya hao 82 walikwa wanaume huku 22 wakiwa maofisa wa kike  kati ya hayo 10  wakitoka  Chuo  cha Mafunzo,  Zanzibar.
Rais  aliahidi  kushughulikia changamoto zinazolikabili jeshi hilo la magereza kabla hajaondoka madarakani na kumwagiza Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja kumwandikia barua Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani mahitaji yao yote ili aweze kuyashughulikia kabla ya kuondoka madarakani.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved