Mbunge wa Viti Maalum CUF, Clara Mwatuka afariki kwa ajali.

mwatuka
Clara Mwatuka enzi za uhai wake.
Aliyekuwa Mbunge wa Viti maalumu kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Clara Mwatuka, amefariki dunia leo Jumapili jioni baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupinduka lilipokuwa linashuka eneo la Makonde Plateu kuelekea Ndanda, Masasi mkoani Mtwara.
mwatuka gari
Gari alilopata nalo ajali marehemu Mwatuka.

Gari ilikuwa inaendeshwa na dereva wake, ambaye inasemekana ni mwanaye. Maiti ya marehemum Mwatuka imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Ndanda.
Viongozi waandamizi wa CUF wamethibitisha kutokea msiba huo.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved