NEC yaandikisha watu milioni 21

Jaji mstaafu Damian Lubuva
   TUME ya Uchaguzi (NEC), imesema imeandikisha zaidi ya watu milioni 21 nchini tangu uandikishaji uanze Februari 23, mwaka huu na kwamba, Dar es Salaam pekee, wameandikishwa watu zaidi ya milioni mbili.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema juzi Dar es Salaam kuwa, uandikishaji wa wapiga kura katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR) unaendelea jijini humo hadi Agosti 8.
Kwa mujibu wa Jaji Lubuva, baada ya siku hizo zilizoongezwa, hakutakuwa na muda mwingine utakaoongezwa.
“Tumieni muda ulioongezwa kujiandikisha, vinginevyo mtaikosa haki yenu ya kupiga kura kwa sababu ya kutoandikishwa katika Daftari la Wapigakura,” Jaji Lubuva alisema.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved