Utumiaji dawa za kulevya waongezeka

MATUMIZI ya dawa za kulevya nchini yameongezeka kwenye mikoa 12 nchini yakionesha dawa aina ya heroini na bangi zikiongoza kwa kutumiwa zaidi.
Utafiti uliofanywa kwenye mikoa 12 nchini iliyopo pembezoni mwa barabara kuu zinazounganisha miji au nchi nyingine, zikiwa kwenye hatari zaidi ya wananchi wake kutumia dawa hizo.
Mikoa hiyo ni Mtwara, Dodoma, Morogoro, Pwani, Kilimanjaro, Tanga, Arusha, Mwanza, Mbeya, Shinyanga, Geita na Kigoma. Wakiwasilisha matokeo ya utafiti huo juzi Dar es Salaam, watafiti waliohusika kwenye kazi hiyo, walisema kazi hiyo ilifanywa kati ya Julai 2013 na Agosti 2014 katika mikoa hiyo.
Mmoja wa watafiti hao, Moza Makumbuli alisema kutoka mikoa hiyo 12, watumiaji wa dawa hizo wanapata shida kubaini aina ya dawa kati ya heroini au kokeni, bali huita dawa hizo unga.
Katika mkoa wa Tanga, utafiti umebaini matumizi ya dawa za kulevya yamesambaa kwenye miji midogo na vijijini nje ya mji kwenye maeneo ya kandokando ya barabara ya Segera,Tanga.
Mkoani Mtwara, utafiti ulionesha watumiaji wa dawa kwa njia ya kujidunga ni wachache ukilinganisha na wavutaji wa dawa hizo kwenye Manispaa ya mkoa huo, lakini pia utafiti umeonesha Mji wa Masasi una watumiaji wa dawa hizo.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved