Walimu Kinondoni kupanda daladala bure

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj7FLm-CLAvrtWhJit9qKVsGNWlRK_47S4sPVVTxqKvVUOtwKxw8LCpSoOA35foQpF2vj12PLEkTKnvZf9MdfOw6k8ZNy3p3R-PIri7YJI6P-LySstMC81DIIPXXd3dmo2YhjGzLEaGM2fp/s1600/makonda.jpg
Dc Paul Makonda akitoa ufafanuzi
Mkuu wa wilaya ya Kinondono DC Paul Makonda ameagiza walimu wote wa shule za serikali kupanda daladala bure, ametoa tamko hilo rasm baada ya kikao na madereva pamoja na wamiliki wa vyombo vya usafiri yaani Darcoboa na Uwadar kwakukubaliana kuto wachaji nauri walimu pia Mh Makonda ameeleza msukumo wake mpaka kufikia hatua hiyo kuwa ni
 Moja, kwa kuzingatia changamoto za nauli za mara kwa mara wanazolazimika kuzilipa walimu ili kuyafikia kwa wakati maeneo yao ya kufanyia kazi 
pili, ni kuhakikisha mimi na serikali yangu ya wilaya ya Kinondoni tunakuwa sehemu ya juhudi za Mheshimiwa Raisi za kuboresha maslahi na mazingira ya walimu ya kufanyia kazi ili matarajio ya ndoto yake anayoipigania usiku na mchana ya kutaka kuiona sekta ya elimu nchini ikikua kwa kasi yanatimia. 

Na tatu, ni kuwafanya walimu wa wilaya ya Kinondoni na Dar es Salaam kwa ujumla kama watumishi wenzangu wa serikali nao wanafaidi sehemu ya matunda ya serikali yao ambayo kwa dhati imedhamiria kubadilisha maisha yao ili na wao waweze kubadilisha maisha ya vijana wetu kupitia taaluma.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved