Wekundu wa Msimbazi wahamishia hasira kwa Singida united na kumchakaza

Jumapili ya February 28 Kombe la FA Tanzania liliendelea kwa klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba kushuka dimbani kucheza mchezo wake wa 16 bora dhidi ya klabu ya Singida United katika dimba la Taifa Dar Es Salaam.
Simba ambao waliingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya kupata majeraha ya kufungwa na Yanga katika mechi zao mbili za Ligi Kuu, wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 5-1, hivyo Simba wametinga hatua ya 8 bora ya Kombe hilo.
Magoli ya Simba yalifungwa na Danny Lyanga dakika ya 3, Hamis Kiiza dakika ya 18 na 66, na Awadh Juma dakika ya 82 na 86, wakati goli pekee la Singida United lilifungwa na Paul Malamla dakika ya 90 ya mchezo.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved