Klabu ya Barcelona imeliomba shirikisho la soka barani ulaya UEFA kutojumuisha jina la kiungo wake wa zamani Luis Figo katika orodha ya wachezaji wake wa zamani ambao walipangwa kushiriki kwenye mchezo wa kirafiki kati ya timu inayoundwa na wachezaji wa zamani wa Juventus na Barcelona dhidi ya timu ya dunia uliopangwa kufanyika wiki hii .
Hatua hii inakuja baada ya mashabiki wa Barca kuandamana wakionyesha hasira zao kwa kitendo cha mchezaji huyo kuihama klabu yao na kujiunga na mahasimu wao kwenye soka la Hispania Real Madrid miaka 15 iliyopita .
Figo kabla ya hapo alicheza kwenye uwanja wa Nou Camp kwa miaka mitano kabla ya kuhamia Santiago Bernabeu mwaka 2000 na kitendo hiki bado hakijasahaulika akilini mwa mashabiki wa Barcelona ambao wameonyesha hisia zao.
Figo akitambulishwa na rais wa Madrid Florentino Perez pamoja na gwiji hayati Alfred Di Stefano mwaka 2000 wakati aliposajiliwa na Real Madrid. |
Figo alichezea klabu hizi mbili kwa kipindi cha miaka kumi kati ya mwaka 1995 na 2005 ambapo alihamia Inter Milan ya Italia .
Hivi karibuni Figo aliingia kwneye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa shirikisho la soka duniani Fifa kabla ya kujitoa kuelekea mwishoni mwa uchaguzi huo .
Chanzo millardayo
No comments:
Post a Comment