Wiki mbili baada ya kumalizika kwa ligi kuu ya Uingereza, dirisha la usajili barani ulaya limeanza kushika hatamu.
Klabu ya Liverpool leo hii imetangaza kukamilisha usajili wa kiungo James Milner kutoka Manchester City.
Milner mwenye umri miaka 29, alipiga chini nafasi ya kuendelea kubaki
Etihad Stadium ili awese kupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha
kwanza chini ya Brendan Rogers msimu ujao.
Milner amemaliza mkataba wake na City, na atajiunga rasmi na Liverpool tarehe 1 mwezi ujao.
Mchezaji huyo alijunga na City akitokea Aston Villa miaka minne
iliyopita na amefanikiwa kutwaa makombe mawili ya Ligi kuu ya Uingereza
pamoja na FA Cup.
No comments:
Post a Comment