Picha za Xavi alivyoagwa Barcelona, hakuweza kuzuia huzuni yake!!



XAVI4

 Kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa kati ya Barcelona dhidi ya Juventus, kiungo Xavi mwenye umri wa miaka 35 alipewa heshima katika klabu ambayo aliitumikia kwa muda mrefu tangu ana umri wa miaka 11 alipojiunga nayo.

XAVI

Fainali hiyo inayosubiriwa na watu wengi itafanyika siku ya Jumamosi.

Xavi ameshindwa kuzuia hisia zake na kumwaga machozi wakati wa shamrashamra za kumuaga ndani ya klabu yake ya Barcelona kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Juventus.



Xavi amemshukuru kocha Luis Enrique kwa kumuwezesha kubaki katika klabu hiyo msimu uliopita huku akishindwa kuvumilia maneno ya Iniesta aliposimama na kumuaga kwa niaba ya wachezaji wenzake.

Kiungo huyo alitangaza mwezi uliopita kwamba anakwenda kumalizia soka yake katika klabu ya Al-Sadd ya Qatar mwishoni mwa msimu, akihitimisha miaka yake 24 kuwa na vigogo hao.
Chanzo millardayo

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved