DRFA YASIKITISHWA NA MATOKEO MABAYA YA TAIFA STARS.


Chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam DRFA,kimesikitishwa na
matokeo mabaya iliyoyapata timu ya taifa (Taifa Stars) kwa kufungwa mabao
3-0 dhidi ya Mafarao wa Misri,katika mchezo wake wa kwanza uliopigwa jana usiku ugenini wa kusaka tiketi ya kushiriki michuano ya kuwania kombe la mataifa ya afrika (AFCON).
Mwenyekiti wachama hicho,Almas Kasongo, amesema matokeo hayo
yamewafadhaisha mno watanzania wenye uchu wa kuona timu hiyo inapata matokeo mazuri yaliyokosekana kwa kipindi kirefu.
Amesema anaamini kuwa kikosi hicho kina wachezaji wazuri na wenye uwezo
lakini wamekuwa wakikosa mbinu za kufanya vizuri kwenye timu ya taifa hasa kwenye safu ya ushambuliaji,ikilinganishwa na uwezo wanaouonesha kwenye michuano ya ligi wakiwa na klabuzao.
Hata hivyo Kasongo amesema licha ya Stars kuanza vibaya katika harakati zake za
kuwania tiketi yamichuano hiyo ya afrika,bado nafasi ipo ya kujipanga upya
kwa kuanza kuangalia uwezo wa benchi la ufundi.
Aidha amesema DRFA inaamini kuwa Tff  inauwezo wa kutafuta mwarobaini wa
kutibu tatizo la matokeo mabaya kwa Starz,bila kumuonea mtu aibu.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved