Madereva wameipongeza serikali kwa utatuaji wa mgogoro wao na wamiliki wa mabasi.

Hatimaye umoja wa madereva umeipongeza serikali kwa hatua yake ya utatuaji wa mgogoro wa kimaslahi kati ya madereva na waajili wao ambapo pia umeahidi kutokugoma tena.
Inatajwa kuwa kikao kilichofanyika june 23 mwaka huu kati ya madereva, serikali na wamiliki wa mabasi ndicho kilichozika mgogoro wa muda mrefu wa kimaslahi ambao ulisababisha uwepo wa migoma ya mara kwa mara.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa katika kikao cha madereva zaidi ya 4000 msemaji wa umoja huo Bw Rashid Saleh anasema hatimaye dereva wa kitanzania amesaminiwa kwa kupatiwa mkataba ambao utamfanya afurahiye kazi yake.
 
Aidha katika mkutano huo pia ambao ulitumika kutangaza uanzishwaji wa chama cha wafanyakazi madereva nchini, madereva walitakiwa kuhakikisha wanakuwa mstali wa mbele katika kuhakikisha maslahi yao yanatekelezeka.
 
Kwa mujibu wa madereva waliozungumza na ITV licha ya kuahidi kufanya kazi hiyo kwa ustadi mkubwa wamesema kuwa rasimu hiyo ya mkataba itawawezesha kukidhi mahitaji yao muhimu ambayo wanadai kuyakosa kwa kipindi cha miaka 50 ya uhuru sasa.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved