Mbunge
wa viti maalum mkoa wa Singida, Diana Chilolo (wa kwanza kushoto)
akipokelewa na kikundi cha uhamasishaji cha Nyota cha Mandewa manispaa
ya Singida. Chilolo alifanya ziara ya kikazi katika manispaa ya Singida
hivi karibuni na kuwataka wanawake kuondoa woga na kujitokeza kwa wingi
kuomba nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu ujao.
Mbunge
wa viti maalum mkoa na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Singida, Diana
Chilolo,akizungumza na wajumbe wa Baraza la UWT Singida vijijini ambapo
aliwataka wahamasishane katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi
kwenye uchaguzi mkuu ujao.Kulia ni katibu wa UWT mkoa Anjela Robert na
kushoto ni Katibu UWT wilaya ya Singida, Hadija Kissuda.
Baadhi
ya wajumbe wa baraza la UWT manispaa ya Singida,wakimsikiliza mbunge wa
viti maalimu na Mwenyekiti wa UWT mkoa, Diana Chilolo wakati
akizungumza nao kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya
wananchi mjini Singida. (DK)
Baadhi
ya wajumbe wa UWT wilaya ya Singida vijijini,wakimsikiliza mbunge wa
viti maalum na mwenyekiti wa UWT mkoa wa Singida,juzi kwenye ukumbi wa
mikutano wa chuo cha wananchi mjini Singida.(Picha na Nathaniel Limu).
MBUNGE
wa viti maalum (CCM) mkoa wa Singida, Mh. Diana Chilolo, amesema katika
kipindi chake cha miaka 15 bungeni, hajawahi kusinzia wala kulala kwa
madai kwamba muda wote amekuwa akisaka kwa udi na uvumba majibu kutoka
serikalini ya kero zinazowasumbua wanawake na wananchi kwa ujumla.
Chilolo
ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) Tainzania mkoa wa
Singida, alisema hayo wakati akizungumza kwenye kikao cha Baraza la UWT
Manispaa ya Singida kilichofanyika kwenye Chuo cha Maendeleo ya
Wananchi mjini hapa.
Akiijengea
nguvu hoja yake hiyo,alisema hatua hiyo ya kutokulala au kusinzia
bungeni, imepelekea awe mwanamke wa kwanza katika kuuliza maswali mengi
ya msingi, hoja na mchango kuanzia mwaka wa 2005 hadi sasa.
“Bungeni
ni mahali pa kuwasilisha kwa nguvu zote kero za wananchi na vilio
mbalimbali, ili serikali iweze kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu, ukisinzia
tu wacha kulala au kuzurura ndani au nje ya bunge, utakuwa hauwatendei
haki wananchi unaowawakilisha bungeni”, alifafanua.
Akisisitiza,
Chilolo alisema bunge lina majukumu mengi makubwa ambayo ni pamoja na
kuhakikisha kwamba nchi inaendeshwa vizuri, huduma zinatolewa kiusahihi
kwa wananchi, na kwamba fedha za wananchi zinatumika vizuri na
zinatolewa maelezo sahihi.
“Kwa
hiyo kuanzia mwaka 2005-2009, utafiti wa uhakika unaonyesha kwamba
nilikuwa mwanamke wa kwanza na mbunge wa nne kati ya wabunge 309 kwa kwa
kujumuisha idadi ya awamu 214 (ushiriki) ambao mbunge aliuliza swali la
msingi, swali la nyongeza au kutoa mchango.
Hapa
nilitanguliwa na aliyekuwa mbunge, Dk.Slaa aliyekuwa na idadi 268,
Mgana Msindai 256 na George Lubeleje 225″, alisema Chilolo.
Alisema
toka kipindi hicho hadi sasa amekuwa akiongoza kwa ujumla wa ushiriki
na kuuliza maswali ya msingi, nyongeza na kutoa michango mbalimbali kwa
manufaa ya wakazi wa mkoa wa Singida na taifa kwa ujumla.
“Utendaji
wangu huo bungeni,nina kila sababu ya kuwaambia au kuwaomba tena ridhaa
mnichague kwa kunipa kura za kutosha kwenye uchaguzi mkuu ujao, ili
niendeleze juhudi za kuwatumikia kwa vile nimeonyesha wazi kwamba uwezo
wa kuwatumikia, ninao wa kutosha”, alisema na kushangiliwa kwa nguvu na
wajumbe.
Kuhusu
watu wanaotoa rushwa ili waweze kupata nafasi ya kugombea nafasi
mbalimbali za uongozi, alisema mwanachama wa UWT anaweza kuchukua kile
anacholazimishwa kupewa kwa madai hiyo ni riziki kwa vile hajaiomba wala
kushawishi apewe kitu kwanza ndio aweze kutoa kura kwa mtoa rushwa.
“Kwa
sababau kura ni siri ya mpiga kura, siku ya kupiga kura wewe fanya
maamuzi yako sahihi chagua kiongozi bora mwenye uwezo na uzoefu wa
kuwatumikia wananchi.
Rushwa sio tu itasababisha uchague bora kiongozi, lakini pia rushwa itauawa chama chetu na jumuiya zake”, alisisitiza Chilolo.
No comments:
Post a Comment