Stars ya Mkwasa yaanza mazoezi

TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars imeanza mazoezi jana kwenye Uwanja wa Boko Veterani kujiandaa na mchezo wa marudiano kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Uganda wiki ijayo, huku wachezaji wawili, Vincent Barnabas na Mudathir Yahya wakiongezwa.
Stars inayonolewa na makocha wazawa, Charles Mkwasa na msaidizi wake Hemed Morocco, itakuwa ikifanya mazoezi asubuhi na jioni uwanjani hapo huku timu ikiweka kambi yake katika hoteli ya Kiromo mjini Bagamoyo.
Wachezaji wote walioitwa wameripoti kambini tangu juzi na jana walifanya mazoezi asubuhi isipokuwa Aggrey Morris ambaye ni majeruhi na nafasi yake imekuchukuliwa na Vicent Andrew (Mtibwa Sugar) na Jonas Mkude aliyekwenda kufanya majaribio Afrika Kusini nafasi yake ikizibwa na Mudathir Yahya (Azam FC).
Katika hatua nyingine, mshambuliaji Rashid Mandawa wa Kagera Sugar ambaye ni mmoja kati ya wachezaji walioitwa kwa mara ya kwanza, amesema amefurahishwa kuitwa kwenye kikosi hicho na kuanza mazoezi vyema.
Mchezaji huyo ni alikuwa mmoja wa wachezaji wengine waliojitokeza jana kwenye kikosi cha timu ya taifa kilichoanza mazoezi jana katika Uwanja wa Boko Veterani, Dar es Salaam.
Mandawa ambaye amehamia Mwadui FC ya Shinyanga akitokea Kagera Sugar ya Missenyi, alisema kwa upande wake inampa moyo na kuwa ni hatua nzuri ya kukuza kipaji chake na kuahidi kufanya makubwa zaidi.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved