WAZIRI wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe ambaye
pia ni Mbunge wa Kyela anayemaliza muda muda wake, ameshinda kura za
maoni katika jimbo hilo akiwabwaga wagombea wenzake tisa waliojitokeza
kuwania nafasi hiyo.Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Katibu wa CCM Wilaya ya Kyela, Eva Degeleki alisema Dk Mwakyembe aliibuka mshindi kwa kujizolea kura 15,516 akifuatiwa na George Mwakalinga aliyeambulia kura 4,905.
Degeleki alisema aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Gabriel Kipija alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 2,301 na wagombea wengine waliofuata na kura zao kwenye mabano walikuwa ni Asajile Mwambambale (994), Vincent Mwamakimbula (881), John Mwaipopo (785), Ackim Mwakipiso (601), Benjamin Mwakasyege (442), Dk Leonard Mwaikambo (283) na Gwakisa Mwandembwa (263).
No comments:
Post a Comment