Uongozi wa klabu ya Yanga umemkabidhi gari mshambuliaji mpya
wa klabu hiyo Malimi Busungu gari aina ya Toyota IST kama makubaliano ya
mkataba katika wake.
“Nashukuru Mungu gari langu nimeshapewa na sasa napiga nalo
misele na ukinikuta kwenye daladala basi nimependa mwenyewe au kuna
tatizo, kazi iliyobaki ni kuthibitisha thamani yangu kwa Yanga,” alisema
Busungu.
Msham,buliaji huyo amejiunga na mabingwa hao wa ligi kuu wiki
chache zilizopita akitokea kwenye klabu ya Mgambo JKT ya jijini Tanga
ambapo alimaliza ligi akiwa mfungaji bora wa klabu yake aliyokuwa
akiitumikia.
No comments:
Post a Comment