Moto ukiwa unawaka katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga
Hapa ni
katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga ambako leo Juni 2,2015 ndiyo
kilele cha maonesho ya bidhaa za viwandani kanda ya ziwa yaliyoandaliwa
na shirika la Viwanda Vidogo nchini SIDO.Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally
Nassoro Rufunga ndiye aliyefunga maonesho hayo yaliyodumu kwa siku 5
yakihusisha wajasiriamali 260 kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Kabla ya kufunga maonesho hayo ambayo yamefanyika mkoani Shinyanga,mkuu wa mkoa huo Ally Rufunga alitembelea mabanda mbalimbali.
Mwanafunzi
Asha Hamis kutoka chuo cha VETA Shinyanga akipanda kwenye mtambo
unaitwa Loader na kuonesha utaalam wake wa kufanya kazi kwa kutumia
mtambo huo,baada ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga kutembelea
banda la chuo cha VETA
Mkuu wa
mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga akimpongeza mwanafunzi wa VETA Asha Hamis
aliyeendesha Loader na mwenzake Jafari ( katikati) aliyeendesha Greda
hapo uwanjani.
No comments:
Post a Comment