MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba
amejiuzulu rasmi wadhifa wake huo ndani ya chama kwa kikle alichokitaja
kuwa ni kukiukwa kwa Katiba ya chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Peacock jijini
Dar es Salaam, Profesa Lipumba amesema UKAWA ilianzishwa kwa lengo la
kusimamia rasimu ya katiba mpya kutokana na maoni ya wananchi "sasa
wenzetu wamegeuza UKAWA kwa kuleta mtu ambaye alishiriki kupitisha
katiba pendekezwa ambayo siyo maoni ya wananchi hivyo kiongozi
atakayeshinda kupitia UKAWA hawezi kusimania maoni ya wananchi ya rasinu
iliyopendekezwa na Warioba," amesema Lipumba.
Cha ajabu ni kwamba wakati wa vikao vya kumpitisha Lowassa kuwa
mgombea wa Ukawa, Profesa Lipumba alikuwepo na ndiye aliyetoa taarifa
kuhusu ujio wa Lowassa, hivyo taarifa hii inakinzana na kile
alichokisema hapo awali. Kujiuzulu huko kunahitimisha wasiwasi wa muda
sasa ndani ya chama chake kuhusu hatima yake kutokana na sababu ambazo
hazikujulikana mara moja.
Profesa Lipumba alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama mwaka 1999 na
kugombea urais katika vipindi viinne ambavyo vyote alishindwa.
Tutawaletea habari kamili hivi punde.
No comments:
Post a Comment