BREAKING NEWS: Profesa Lipumba ajiuzulu rasmi Uenyekiti CUF

  MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amejiuzulu rasmi wadhifa wake huo ndani ya chama kwa kikle alichokitaja kuwa ni kukiukwa kwa Katiba ya chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam, Profesa Lipumba amesema UKAWA ilianzishwa kwa lengo la kusimamia rasimu ya katiba mpya kutokana na maoni ya wananchi "sasa wenzetu wamegeuza UKAWA kwa kuleta mtu ambaye alishiriki kupitisha katiba pendekezwa ambayo siyo maoni ya wananchi hivyo kiongozi atakayeshinda kupitia UKAWA hawezi kusimania maoni ya wananchi ya rasinu iliyopendekezwa na Warioba," amesema Lipumba.
Cha ajabu ni kwamba wakati wa vikao vya kumpitisha Lowassa kuwa mgombea wa Ukawa, Profesa Lipumba alikuwepo na ndiye aliyetoa taarifa kuhusu ujio wa Lowassa, hivyo taarifa hii inakinzana na kile alichokisema hapo awali. Kujiuzulu huko kunahitimisha wasiwasi wa muda sasa ndani ya chama chake kuhusu hatima yake kutokana na sababu ambazo hazikujulikana mara moja.
Profesa Lipumba alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama mwaka 1999 na kugombea urais katika vipindi viinne ambavyo vyote alishindwa.
Tutawaletea habari kamili hivi punde.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved