Yanga wamuuza Sherman

  KLABU ya soka ya Yanga imefanikiwa kumuuza kwa mkataba wa miaka mitatu mshambuliaji wake raia wa Liberia, Kpah Sherman aliyejiunga na timu ya Mpumalanga Black Aces iliyopanda kucheza Ligi Kuu ya Afrika Kusini ya PSL msimu huu.
Sherman alilazimika kuondoka nchini wiki iliyopita na kuiacha timu yake Yanga ikiwa kwenye michuano ya Kombe la Kagame kwa ajili ya kukamilisha vipimo vya afya na makubaliano ya kimaslahi kabla ya kusaini kuichezea timu hiyo.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina gazetini kwa kuwa sio msemaji wa timu, mmoja wa viongozi wa nafasi za juu kwenye klabu hiyo alisema wamemuuza Sherman kwa dola 150,000 sawa na zaidi ya Sh milioni 300, ambapo klabu hiyo inatarajia kutuma fedha hizo wakati wowote baada ya kukamilika kwa taratibu za uhamisho wake.
“Ni kweli Sherman amefuzu vipimo vya afya na kusajiliwa kwa mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Mpumalanga Black Aces, kila kitu kinakwenda vizuri na sasa tunamalizia taratibu za uhamisho wake ili wenzetu waweze kututumia malipo yetu tuweze kuyatumia kwa kuziba pengo la Sherman katika siku mbili zilizobaki kwenye usajili wetu,” alisema kiongozi huyo.
Kiongozi huyo alisema kuondoka kwa Sherman ni pengo kubwa kwa timu yao kwa sababu ndiyo kwanza alianza kuzoea Ligi ya Tanzania baada ya kuanza vibaya msimu wake wa kwanza lakini anaamini atafanikiwa huko anakokwenda na wao wapambana kuhakikisha wanamtafuta mtu sahihi wa kuziba nafasi yake.
“Alikuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi cha Yanga lakini siku zote mpira haupo kwa ajili ya burudani na biashara, pia ndiyo maana tumemruhusu kuondoka na sisi tumepata pesa ambazo tutazitumia kuhakikisha tunaimarisha kikosi chetu katika sehemu ambazo tumeona zinamapungufu,” alisema kiongozi huyo.
Sherman alitua Yanga kwenye dirisha dogo la usajili msimu uliopita na kuonesha kiwango cha juu kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe, lakini baada ya hapo alionekana kushuka kiwango na kupoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza licha kumaliza msimu akifunga mabao sita kwenye ligi katika mechi 16 alizocheza mzunguko wa pili huku akijivunia ubingwa wa ligi ya Tanzania Bara msimu uliopita.
kuwa Musonye alikuwa akiipendelea timu hiyo licha ya kugoma kuingia katika vyumba vya kubadilishia nguo, ambapo tayari timu hiyo ilishaonywa huko nyuma kwa kitendo kama hicho. Timu hiyo juzi iligoma tena kuingia katika vyumba vya kubadilishia nguo wakati wa mchezo wa fainali ya Kagame dhidi ya Azam FC, ambao walifungwa 2-0 na kushindwa kutwaa taji hilo.
Wakizungumza na waandishi kwa nyakati tofauti kuhusu ugomvi wao, viongozi wote wawili walikiri kushikana mashati, huku Musonye akisema lazima wawekeane heshima. Musonye hakusema sababu ya wao kushindwa kuelewana akijitetea kuwa katika masuala ya soka, kusuguana ni jambo la kawaida, hivyo walikuwa wakiwekeana heshima. “Tumeshayamaliza ilikuwa ni jambo dogo tunawekeana heshima. Kwenye soka mambo ndivyo yalivyo,”alisema.
Mgoi aliweka bayana kuwa Musonye alikuwa akitaka mgeni rasmi wa mashindano hayo awe Odinga ambaye alikuwa uwanjani hapo kushuhudia fainali za Gor Mahia na Azam. Alisema TFF haikuwa na taarifa kutoka serikalini kuwa Odinga atakuwa nchini kwa ajili hiyo, hivyo tayari walimuandaa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki kuwa mgeni rasmi.
Alisema baada ya TFF kuweka msimamo wao kama waandaaji wa mashindano kwa mgeni wao ambaye ni Sadiki, Musonye alianza kutoa maneno makali na kuanzisha vurugu. Hatahivyo, kama ilivyopangwa na TFF, Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaam ndiye aliyetoa zawadi kwa Azam ambao ni mabingwa wapya wa Afrika Mashariki na Kati.
Pamoja na hilo, Mgoi alisema Musonye alikuwa akionesha upendeleo dhidi ya timu hiyo ya Kenya akiitetea timu ya Gor Mahia ambayo ilikiuka onyo ililopewa awali la kutoingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kwa imani za kishirikina.
Alisema timu hiyo ilivunja kitasa katika sehemu ambazo walikatazwa awali kuingia, na wao kutumia nguvu na kufanya lolote kwa vile tu walikuwa wakitetewa na katibu huyo wa Cecafa.
“Gor Mahia imekuwa na dosari nyingi ikiamini haiwezi kufanywa lolote na tunapomshirikisha Musonye hakutoa ushirikiano na badala yake amekuwa mtu wa kuitetea, ndio maana alipoonesha upendeleo wake, nasi tulisimama kuonesha uzalendo wetu,”alisema na kuongeza kuwa, timu hiyo imekuwa ikifanya uharibifu ikisaidiwa na kituo kilichokuwa kinarusha matangazo ya soka cha Supersport.
Kitendo hicho cha Gor Mahia kutoingia katika vyumba vya kubadilisha nguo sio cha kwanza, kwani katika mchezo dhidi ya Yanga walipita katika sehemu ambapo hupaki magari ya kurusha matangazo ya soka kwenye televisheni na kupewa onyo la kutorudia.

No comments:

Post a Comment

©2015 New Day Pro Media.All Rights Reserved